<sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
<noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>

    久久精品蜜芽国产亚洲av,国产成人观看免费全部完,1024综综合合久久AV,午夜国产成人精品,国产精品综合承认,国产高跟黑色丝袜在线

    Mapato ya mauzo ya nje ya chai nchini Kenya yaongezeka kwa asilimia 18 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2024

    (Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 27, 2024

    Mkulima wa chai akionyesha majani ya chai ya zambarau yaliyochumwa punde kwenye shamba la chai ya zambarau katika Kaunti ya Muranga, Kenya, Mei 6, 2024. (Xinhua/Han Xu)

    Mkulima wa chai akionyesha majani ya chai ya zambarau yaliyochumwa punde kwenye shamba la chai ya zambarau katika Kaunti ya Muranga, Kenya, Mei 6, 2024. (Xinhua/Han Xu)

    NAIROBI - Mapato ya mauzo ya nje ya chai nchini Kenya yameongezeka kwa asilimia 18 katika nusu ya kwanza ya Mwaka 2024, ikichangiwa na ongezeko la usafirishaji wa chai katika masoko muhimu, Idara ya Kiaifa ya Takwimu ya Kenya (KNBS) imesema Jumatano.

    Katika ripoti yake ya kiuchumi, KNBS imesema mapato hayo yalipanda hadi shilingi bilioni 102.4 (kama dola milioni 795 za Kimarekani) kwa kipindi kinachoishia cha mwezi Juni, huku nchi hiyo ikiwa imeuza nje tani 320,563 za chai. Hii inamaanisha ongezeko kubwa kutoka dola milioni 674.9 zilizopatikana kutokana na kuuza chai ya tani 270,287 katika kipindi kama hicho mwaka 2023.

    Mwezi Machi ulirekodi shehena za juu zaidi, ukiwa na chai ya tani 59,599 iliyosafirishwa kuuzwa nje ya nchi, huku mwezi wa Juni ukishuhudia kiwango cha chini zaidi, ukiwa na mauzo ya chai yenye uzito wa tani za metriki 42,894. Kenya ilikuwa na wastani wa mapato ya dola milioni 132 kwa mwezi katika kipindi hicho, KNBS imeeleza.

    Bodi ya Chai ya Kenya, katika ripoti ya hivi karibuni, kuongezeka kwa usafirishaji huo wa chai kunatokana na kufufuka kwa masoko muhimu baada ya kudorora kwa uchumi wa dunia kulikosababishwa na mgogoro wa Russia na Ukraine.

    Wavunaji wakichuma majani freshi ya chai kwenye shamba la chai karibu na Nairobi, mji mkuu wa Kenya, Mei 4, 2023. (Xinhua/Wang Guansen)

    Wavunaji wakichuma majani freshi ya chai kwenye shamba la chai karibu na Nairobi, mji mkuu wa Kenya, Mei 4, 2023. (Xinhua/Wang Guansen)

    Masoko ya msingi ya chai ya Kenya ni pamoja na Pakistan, Misri, Uingereza, Russia na Saudi Arabia, huku masoko yanayoibukia kama vile Chad, Sudan Kusini, Kyrgyzstan, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ethiopia, Azerbaijan, Georgia, Morocco, Angola na Tajikistan pia yakichangia ukuaji.

    Nchi hiyo inazidi kulifanya soko lake kutegemea nchi mbalimbali kwa kupanua soko lake hadi China, ambako hivi karibuni ilifungua kituo cha biashara ili kuwezesha usambazaji wa chai ya Kenya.

    Chai inaendelea kuwa miongoni mwa mambo yanayoipa fedha nyingi za kigeni Kenya, pamoja na shughuli za utalii na kilimo cha bustani. Mwaka 2023, nchi hiyo ya Afrika Mashariki ilipata dola bilioni 1.4 kutokana na mauzo ya chai.?

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

    Picha

    久久精品蜜芽国产亚洲av
    <sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
    <noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>